Serikali mkoani Mwanza imezindua mkakati wa kuhakikisha inawaondoa watoto wanaoishi katika mazingira magumu mkoani humo.
Akizungumza katika uzinduzi wa mkakati huo mkuu wa mkoa wa Mwanza Said Mtanda amesema miongoni mwa mikakati iliyopo ni serikali za mitaa kuhakikisha zinaweka utaratibu wa kuwatambua Watoto waliotoroka katika maeneo yao ikiwa ni Pamoja na wazazi ambao hawatimizi wajibu wao kuchukuliwa hatua kali za kisheria.
Kwa upande wake msimamizi wa huduma za ustawi wa jamii mkoani Mwanza Baraka Makona amesema mkakati huo utatekelezwa katika halmashauri zote 8 za mkoa huu wa Mwanza.
Akizungumza kwa niaba ya wamiliki wa Day care lina Roman amesema jukumu walilonalo hivi sasa nikuhakikisha wanashirikiana na serikali kutokomeza suala hilo .
0 Comments