Boda boda na samia mkoa wa mwanza wamefanya maandamano ya kushtukiza kuelekea kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya ya nyamagana kwa ajili ya kwenda kumuelezea nia yao kwa nchi ya Tanzania na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt samia Suluhu Hassan kwa namna anavyotekeleza miradi ya kimkakati .
Akizungumza mara baada yakufika kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya ya nyamagana mwenyekiti wa boda boda na samia Ramadhan Musabi ameeleza niya yao ya kile kilichopelekea kufanya kufanya maandamano hayo ya kwenda kwa mkuu wa wilaya ya nyamagana.
Nae mkuu wa wilaya ya nyamagana Amina makilagi baada ya kuwapokea boda boda boda hao ameeleza furaha yake na kuwashukuru kwa nia yao ya dhati huku akiwaahidi kuungananao katika harakati zao zote za kuzunguukia miradi mikubwa yote iliyopo hapa mkoani mwanza.
0 Comments