Header Ads Widget

Responsive Advertisement

USHIRIKIANO WA ZANZIBAR NA OMAN KUENDELEZA KUIMARIKA KATIKA NYANJA MBALI MBALI

 

Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendeleza ushirikiano na Serikali ya Oman katika nyanja mbali mbali ili kuziletea nchi hizo maendeleo.


Ameyasema hayo Ofisini kwake Mazizini Wilaya ya magharibi B wakati alipokuwa akizungumza na mjumbe kutoka Serikali ya Oman Sheikh Abdullwahab Suleiman alipomtambulisha kuwepo Zanzibar kwa ajili ya kufundisha elimu ya mwezi, nyota na sayari nyengine.


Amesema ni muhimu kwa maulamaa kufahamu elimu hiyo katika kuwasaidia kuzitambua vyema sayari na mwenendo wake ambapo elimu hiyo ina manufaa wakati wa muandamo wa mwezi.


Aidha, Mufti huyo aliwataka Maulamaa hao kuzingatia kwa umakini na kuifahamu elimu hiyo, kwani itawaletea Wazanzibari manufaa kujua masuala ya sayari.


Nae Mtaalam wa maswala ya nyota kutoka Oman Sheikh Abdullwahabi Suleiman amesema ujio wake huo Zanzibar una lengo la kutoa elimu kwa Maulamaa pamoja na Mashekh kutoka Ofisi ya Mufti ili kuweza kufahamu elimu hiyo.


Pia ameishukuru Ofisi ya Mufti mkuu wa Zanzibar kwa mapokezi mazuri ambayo yataleta mshikamano baina ya Serikali hizo kwani Zanzibar na Oman wanaudugu wa muda mrefu.


Mtaalam wa maswala ya nyota na sayari Sheikh Abdulwahabi yupo Zanzibar kwa muda wa wiki moja kwa lengo la kutoa elimu hiyo.

Post a Comment

0 Comments