NJE SPORTS YATINGA ROBO FAINALI KWA KISHINDO, YAILAZA TPDC 36-23

 

Timu ya netiboli ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (NJE Sports) imeendelea kung’ara katika michezo ya Mei Mosi kwa kuibuka na ushindi wa mabao 36-23 dhidi ya TPDC, katika mchezo uliopigwa kwenye viwanja vya Mwenge, mkoani Singida.


Mchezo huo ulianza kwa kasi, huku NJE Sports wakionyesha ubora wa hali ya juu na kumaliza kipindi cha kwanza wakiongoza kwa mabao 19-13. Kipindi cha pili walizidi kuimarika, wakiboresha safu ya ulinzi na kushambulia kwa ufanisi zaidi.


Akizungumza baada ya mchezo, Kocha wa NJE Sports, Bw. Mathew Kambona, amewapongeza wachezaji wake kwa kujituma na kufuata maelekezo. “Tunajipanga upya kwa hatua inayofuata, tukilenga kuongeza kasi na nidhamu ya ushindi,” alisema.


Kwa matokeo hayo, NJE Sports imefuzu rasmi hatua ya robo fainali katika mashindano hayo ya kitaifa yanayoshirikisha timu kutoka wizara na taasisi mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani.

Post a Comment

Previous Post Next Post