Header Ads Widget

Responsive Advertisement

NJE SPORTS YAICHAPA WIZARA YA UJENZI 1-0 KATIKA MCHEZO WA KIRAFIKI SINGIDA



Timu ya mpira wa miguu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Nje Sports) imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya timu ya Wizara ya Ujenzi katika mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye Uwanja wa Mwenge, mkoani Singida.


Mchezo huo, ambao ulikuwa na ushindani mkubwa na nidhamu ya hali ya juu kutoka kwa timu zote mbili, ulikuwa sehemu ya maandalizi kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, yanayotarajiwa kufanyika Mei Mosi, 2025.


Bao pekee la Nje Sports lilifungwa katika kipindi cha pili na mshambuliaji Juma Jongo, aliyepokea pasi safi kutoka kwa kiungo Mukrim, baada ya shambulizi la pamoja lililotokana na umiliki mzuri wa mpira katikati ya uwanja.


Licha ya juhudi za Wizara ya Ujenzi kusawazisha bao hilo, safu ya ulinzi ya Nje Sports ilionyesha uimara mkubwa, huku kipa wao Adam Mlele akiokoa michomo kadhaa ya hatari na kudhihirisha uwezo mkubwa langoni.


Timu hizo zipo mkoani Singida kushiriki michezo mbalimbali ikiwa ni sehemu ya shamrashamra za kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) mwaka huu.

Post a Comment

0 Comments