Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Mbeto: Haki ya wananchi kushiriki uchaguzi isiporwe na Vyama vya Siasa


 

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar


Chama cha Mapinduzi (CCM)  kimesifu kupevuka kwa  maono ya  kisiasa  yalioonyeshwa na Kiongozi wa ACT  Wazalendo, Dorothy  Semu ,aliyeitangazia dunia  chama chake kitashiriki uchaguzi  Mkuu oktoba  mwaka huu bila  longolongo.


Pia CCM  kimebaini kuwepo  tofauti  ya uelewa, upeo, busara  na ufahamu  kati ya Kiongozi wa ACT  na Mwenyekiti  wake  Othman  Masoud Othman .


Hayo yameelezwa na Katibu wa Kamati  Maalum  ya NEC Zanzibar,  Idara  ya itikadi , Uenezi na Mafunzo ,Khamis  Mbeto  Khamis,  aliyesema kwa chama makini  ni aibu kukimbia  uchaguzi wa kidemokrasia.  


Mbeto  alisema haki ya kushiriki  uchaguzi inawahusu  zaidi  wananchi kupitia  vyama vyao  lakini  si halali kwa viongozi wa Vyama vya siasa  kuwazuia wananchi wasitumie  haki na wajibu wa kuchagua au kuchaguliwa.


Alisema si hivyo  tu ,bali kiongozi  wa ACT Wazalendo amezungumza mambo ua msingi  akitumia lugha  komavu ,maneno  yenye hekima na busara,  tofauti na matamshi holela yanayokuwa yakitolewa mara kwa mara na Mwenyekiti  wake.


"Viongozi wa Vyama vya Siasa wasipore madaraka na  haki za wananchi  Waache  kuwazuia ili wasishiriki chaguzi  za kidemokrasia. Haki za vyama zisikwapue matakwa ya  kisheria na kikatiba ya wananchi  na kugeuza  miliki ya viongozi wa vyama " Alisema Mbeto 


Aidha  Katibu  huyo Mwenezi  alisema  maelezo  alioyatoa kiongozi wa ACT Wazalendo,  hayakuambatana kabisa na maneno ya   vitisho au yenye   kujenga hofu na taharuki katika  jamii .


"Kiongozi wa ACT amejenga hoja  zake  bila kutumia  lugha  ya ubabe tofauti na Mwenyekiti wake .Hii ni tofauti iliopo kati ya Mwenyekiti na kiongozi  wa chama. Ama kweli maarifa ya  kinamama huwazidi baadhi ya kinababa ' Alieleza


Hata hivyo,  katika maelezo yake, Mbeto  akimtaka Semu afute  ndoto za ACT kukishikda CCM kwakuwa hakijapata  uwezo huo  na wananchi hawajawa tayari  kukiamini  ACT ili kuiongoza Zanzibar.


Pia  Mbeto  alisema chini ya usimamizi wa  Tume ya Uchaguzi  Zanzibar  na Tume huru ya Uchaguzi  Tanzania, vyama vya  upinzani  vimekuwa vikishinda na kupata viti vingi ikiwemo  kura za urais .


"Ni masikitiko kwa ACT  Wazalendo  kumsimamisha  Othman kuwania nafasi ya urais ili ashindane na mgombea wa CCM Rais Dk Huseein  Ali  Mwinyi. Tunakwenda kushinda mapema asubuhi kweupe" Alisema Mbeto 


Katibu   huyo Mwenezi  alisema  kulingana na kazi kubwa ilofanywa na Serikali  ya awamu ya nane, CCM kina kazi nyepesi mno ifikapo oktoba  mwaka huu.

Post a Comment

0 Comments