BREAKING: Rais wa Burkina Faso Kapteni Ibrahim Traoré amenunua Graders zaidi ya 1,000 na magari mbalimbali ili kusaidia juhudi za ujenzi wa barabara kote Nchini Burkina Faso.
Jana, alikabidhi rasmi mitambo hiyo kwa timu zinazohusika na maendeleo na matengenezo ya miundombinu ya barabara nchini humo
Katika hotuba yake, Captain Traoré alisisitiza umuhimu wa kuwa na barabara bora kutoka mashambani hadi sokoni, akieleza kuwa barabara nzuri zitawawezesha wakulima kusafirisha mazao yao kwenda mijini kwa ufanisi zaidi na bila kuharibika.
Uwekezaji huu mkubwa katika maendeleo ya kitaifa unafanyika licha ya shutuma za awali kutoka kwa Jenerali Langley, ambaye ni Mkuu wa Jeshi la Marekani Kamandi ya Afrika ambaye alidai kuwa Traoré anatumia vibaya akiba ya dhahabu ya nchi ya Burkina Faso kwa manufaa yake binafsi.
0 Comments