Header Ads Widget

Responsive Advertisement

KUELEKEA MAADHIMISHO MALIKALE,MAKUMBUSHO YABAINISHA MAFANIKIO YAKE

Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Dkt Noel Lwoga wakati akizungumza ofisini kwake jijini Dar es salaam akielezea katika kuelekea maadhimisho ya siku ya Siku ya Kimataifa ya Malikale ambayo hufanyika tar 18 April ya kila mwaka.

........................

NA MUSSA KHALID

Taasisi ya Makumbusho ya Taifa la Tanzania imeisisitiza jamii kuendelea kushiriki kikamilifu katika kuhifadhi malikale zilizopo nchini ili kuepukana na madhara yanayosababishwa na majanga na migogoro katika sekta hiyo.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Dkt Noel Lwoga wakati akizungumzia kuhusu  kuelekeza maadhimisho ya siku ya Siku ya Kimataifa ya Malikale ambayo hufanyika tar 18 April ya kila mwaka.

Dkt Lwoga amesema kuwa lengo la kufanyika maadhimisho hayo ni kuhamasisha jamii kutambua umuhimu wa malikale katika maisha yao sambamba na kushiriki katika uhifadhi wa malikale kwa faida ya jamii hiyo.

‘Kwa mwaka huu 2025 maadhimisho haya kauli mbiu kubwa ni kuangazia madhara ya majanga na migogoro katika maeneo ya Malikale lakini pia kutafakari miaka sitini ya utekelezaji wa baraza la kimataifa la Malikale katika kutatua migogoro ya malikale na kushughulikia majanga yanayoathiri malikale hizo”

Aidha Dkt Lwoga amesema mambo yanayoathiri Malikale ni pamoja na mabadiliko ya hali ya hewa ikiwemo maeneo ya bahari yakiongezeka kina na kuleta madhara kwenye malikalie pia kuna madhara ya nayosabishwa na majanga ya asili kama vile mafuriko.

Vilevile kwa shughuli za binadamu pia zimekua zikiathiri Malikale kwa watu kuvamia baadhi ya maeneo na kubomoa jambo linalosababisha kukosa uwepo wa ushahidi wa eneo hilo la kihistoria.

Dkt Lwoga amewasisitiza watanzania kutambua na kuhifadhi vitu vya kale ili kusaidia vizazi vya sasa na vya baadae huku akihamasisha jamii kuanzisha makumbusho binafsi.

Kuhusu Mafanikio ya Makumbusho amesema kwa sasa  wageni zaidi laki mbili wanazitembelea Makumbusho ya Taifa pamoja na maeneo ya Malikale ili kujifunza na kuelewa historia ya nchi yao.

 

Post a Comment

0 Comments