.jpeg)
.jpeg)
NA MUSSA KHALID
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya
(DCEA) imekamata Kilogram 4,568 za dawa mbalimbali za kulevya na kuteketeza
ekari 178 za mashamba ya bangi pamoja na kushikilia magari,pikipiki tano na
bajaji moja vilivyohusika kwenye uhalifu huo.
Pia imefanikiwa kuzuia tani 14 za kemikali bashirifu
zilizokuwa ziingizwe nchini kinyume na sheria pamoja na pakti 10 za pipi zenye
uzito wa gramu 174.77
Hayo yameelezwa jijini Dar es salaam na Kamishna
Jenerali wa Mamlaka hiyo Aretas Lyimo wakati akitoa taarifa kuhusu operesheni ya
Mwezi machi hadi April mwaka huu ambayo wameifanya kwa kushirikiana na vyombo
vingine vya dola katika mikoa ya Dar es salaam,Shinyanga,Tabora,Songwe,Mbeya na
Arusha.
Kamishna Lyimo amesema kuwa katika operesheni
zilizofanyika mkoani Mbeya,raia wa Uganda Herbert Kawalya mwenye hati ya
kusafiria Na.B00132399 na mmiliki wa
Kampuni ya Hoxx Wells Lux Tour Limo alikamatwa akiwa na pakti 10 za pipi zenye
uzito wa gramu 174.77 zilizotengenezwa kwa dawa aina ya bangi yenye kiwango kikubwa
cha sumu ya tetrahydrocannabinol (THC).
“Aidha katika tukio lingine Mkoani Mbeya zilikamatwa
kilogram 1658 za bangi aina ya skanka na kilogram 128.7 za bangi zilizokuwa
zinaingizwa nchini kutoka Malawi’amesema Kamishna Lyimo
Ameendelea kusema kuwa katika operesheni
waliyoifanya jijini Dar es salaam,zilifanikisha ukamataji wa kilogram 220.67 za
bangi aina ya skanka katika kata yaChanika zikiwa zimefichwa chooni huku
kilogram 11 zikikamatwa eneo la ukaguzi wa mizigo kwenye bandari ya kuelekea Zanzibar
“Katika operesheni zilizofanyika mikoa ya
Arusha,Tanga na Manyara zilikamatwa Kilogram 733.74 za dawa za kulenya aina ya
Methamphetamine,kilogram 91.61 za heroin,kilogram 692.84 za mirungi iliyokuwa
inaingizwa kutokea nchini Kenya na Kilogram 115.05 za bangi pamoja na
kuteketeza ekari mbili za mashamba ya bangi’amesema Kamishna Lyimo
Vilevile Kamisha Lyimo amesema katika operesheni
zilizofanyika Wilaya ya Uyui na Nzega mkoani Tabora,Kilogram 845 za bangi
zilikamatwa na ekari za mashamba ya bangi ziliteketezwa.
Katika hatua nyingie Kamishna Jenerali Lyimo ametoa
wito kwa watendaji wa serikali za mitaa kudhibiti uhalifu huo katika maeneo yao
na watachukuliwa hatua endapo watashindwa kukomesha na wakibainika kuhusika
katika uhalifu huo.
Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi Malalamiko
kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU ) Thobias Ndaro
amesema watahakikisha wanafuatilia kwa umakini watumishi wa umma ambao
wanachangia au kuenea kwa changamoto ya dawa za kulenya nchini.
Ametumia fursa hiyo kutoa wito wa watumishi wa umma
kuwa waadilifu kwa kutochangia madawa ya kulevya kushamiri katika maeneo yao.
Hata hivyo wazazi na walezi mnahimizwa kuwa makini
na kufuatilia kwa karibu mienendo ya watoto wenu ikiwa ni pamoja na kuwaasa
wajiepushe na mazingira na sababu zozote zinazoweza kuwaingiza kwenye matumizi
ya dawa za kulevya.