Header Ads Widget

Responsive Advertisement

CCM:Jina la Sheikh Abeid Amani Karume limebaki midomoni mwa wazanzibari wazalendo

 

 

Na Mwandishi  Maalum  , Zanzibar 


Chama Cha Mapinduzi  (CCM ) kimesema kitaendelea kuenzi yale yote yalioanzishwa katika utawala wa Awamu ya Kwanza  chini ya uongozi wa  Rais Hayati Mzee Abeid  Amani  Karume  aliyeuwawa kikatili  Aprili  7 mwaka 1972.


Pia chama hicho bado  kimeahidi   kuwa  kilichokufa ni kiwiliwili cha Mzee  Karume lakini fikra,upeo , vitendo na maono  yake yataendelezwa toka kizazi  hadi kizazi.


Msimamo  huo umetolewa na Katibu  wa Kamati  Maalum  ya NEC  Zanzibar  ,Idara ya Itikadi  , Uenezi na Mafunzo, Khamisi  Mbeto  Khamis , aliyesema  kifo cha Mzee Karume  miaka  53 iliopita,  kimeacha masikitiko na majonzi makubwa.


Mbeto  alisema CCM  kinaamini kuwa  kundi la Wapinga Mapinduzi  Matukufu na maharamia wa madaraka , ndio waliosuka njama za kukatisha maisha  ya kiongozi huyo na kuuridisha   nyuma maendeleo ya Zanzibar     .


Alisema kifo cha kiongozi huyo  jasiri na shupavu, kitaendelea kukumbukwa na kila mzanzibari  kutokana  na uwezo ,upeo na maono ya mbali aliojaliwa kuwa nayo  kiongozi  huyo mzalendo .


"CCM  inaahidi kuendelea kuenzi fikra,  Sera na mikakati  iliotumika katika  Awamu ya kwanza yaliowaletea wananchi maendeleo chini ya  ASP. Tuna jukumu la kuendeleza na kusimamia mema yote  kutekelezwa na kuendelezwa " Alisisitiza 


Aidha aliwahimiza wananachi wa zanzibar kutoacha kumuombea  duwa kwa mungu  Kiongozi  huy azidi kumpa makaazi mema huko aliko na kumsamehe makosa yake  yote.


"Alikuwa kiongozi shujaa na shupavu aliyewewaunganisha wazanzibari  tokea enzi za African  Association Mwaka 1935 hadi kilipoundwa ASP  mwaka 1957 .Lakini pia ndiye   Jemedari Mkuu wa Mapinduzi Zanzibar Januari  Mwaka 1964' Alieleza 


Katibu  huyo Mwenezi  alisema mema aliofanywa na serikali  ya  Mzee  Karume  katika uongozi wake wa miaka nane, yatazidi kukumbukwa na wananachi wa Zanzibar lakini  pia  kwa  kuanzisha mchakato uliounda  Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania  April  26 mwaka 1964 miaka 61 iliopita .


"Hatuwezi kuzungumzia Muungano wa Tanganyika na Zanzibar   na kusahau  sera na juhudi  za  vyama vya ASP  na TANU. Uamuzi wa waasisi   wawili wa mataifa  yetu  Hayati  Sheikh  Abeid Karume na mwenzake Marehemu  Mwalimu Julius  Nyerere utaendelea kuenziwa "Alisema Katibu  huyo Mwenezi 


Kadhalika aliongeza kusema  pamoja na miaka 53 kupita  tokea Kiongozi  huyo alipouawawa na genge la wapinga Mapinduzi, jina lake  halijatoka midomoni mwa wazanzibari  Wazalendo.

Post a Comment

0 Comments