Header Ads Widget

Responsive Advertisement

RAIS MWINYI:TUISHI KWA KUFUATA MISINGI YA UISLAMU


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt, Hussein Ali Mwinyi amewahimiza Waumini wa Dini ya Kiislamu  Kuishi kwa kuifuata Miongozo ya  Uislamu pamoja na kufungamana na Ibada.


Rais Dkt.Mwinyi  amesema hayo alipozungumza katika Mashindano ya Tajwiid Quraan yalioandaliwa na Taasisi ya AlHikma Quraan Foundation yàliofanyika Masjid Jamiu Zenjibar Mazizini Wilaya ya Mjini.


Aidha Rais Dkt, Mwinyi amesema Kazi kubwa inayofanywa na Masheikh na Walimu wa Madarasa ya kuwasomesha Vijana na Kuwa na Uwezo wa Kuhifadhi Quraan inapaswa kuungwa Mkono na kila Mmoja .

Amewanasihi Waislamu kushughulika na Miongozo ya Dini hiyo  ili Wapate kuongoka kwani Quraan ni kitabu cha Uongofu.


Rais Dkt, Mwinyi amewahimiza Waislamu kuzidisha bidii ya  kuisoma Quraan na Kuwasimamia Watoto kuwa na Mwenendo Mzuri unaonekana  wakati wa Mwezi wa Ramadhani .

Halikadhalika Rais Dkt.Mwinyi amewapongeza Wadhamini wanaoendelea  kuyafadhili Mashindano hayo kila Mwaka na  kuwaomba wengine wapya kujitokeza kuunga Mkono Juhudi hizo.

Post a Comment

0 Comments