Siku chache zilizopita Rais wa klabu ya Yanga Hersi Saidi alikuwa nchini Morocco yaliko makao makuu ya CAF kusaini mkataba wa ushirikiano baina ya CAF pamoja na Chama cha vilabu Afrika (ACA) akiwa kama mwenyekiti wa chama hicho cha vilabu.
Lakini pia Raisi Hersi aliungana na Raisi wa TFF Wallace Karia wakati wa uchaguzi wa mkuu wa CAF na Patrick Motsepe kuchaguliwa kwa mara ya pili kuwa raisi wakati Wallace Karia akichaguliwa kuwa mjumbe wa kamati kuu ya CAF. Kwa matukio haya Tanzania tunaendelea kupeperusha vyema bendera ya Soka
Kwani raisi wa Yanga yuko wapi
Wakati nchi nzima ikilaani na kulalamikia maamuzi ya Bodi ya Ligi kuahirisha mchezo baina ya Yanga na Simba uliopangwa kufanyika tarehe 8 machi mambo ni tofauti kwa raisi wa klabu ya Yanga Hersi Said. Kwanza hajatoa tamko lolote mpaka sasa kuzungumzia tukio hilo na mchezo huo pili yupo nchini Hispania akiendelea na majukumu yake ya Shughuli za usimamiaji wa chama cha vilabu Afrika (Africa Clubs Association) akiwa yeye ndiye mwenyekiti.
Haya ni maendeleo makubwa kwa soka letu na uweledi wa viongozi hawa umeendelea kuinua soka letu la Tanzania
Rais Hersi Saidi ameutumia mtandao wake kwa kuandika haya
''Kama Mwenyekiti wa Chama cha Vilabu vya Kiafrika, kuhudhuria hafla ya Jumuiya ya Vilabu ya Ulaya huko Madrid sio tu heshima bali ni fursa muhimu ya kujifunza na kuunganishwa na vilabu vya Uropa.
Kushirikiana na washikadau wakuu katika jumuiya ya soka huturuhusu kubadilishana mawazo, mbinu bora, na mikakati bunifu inayoweza kuinua vilabu na michezo yetu katika bara la Afrika.
Kwa pamoja, tunaweza kukuza ushirikiano, kuongeza ukuaji, na kuhamasisha kizazi kijacho cha vipaji vya soka. Furahi kwa majadiliano mbele!''
ACA kukutana na ECA!
0 Comments