Header Ads Widget

Responsive Advertisement

DKT. NCHEMBA ASHIRIKI MKUTANO WA 50 WA BODI YA WADHAMINI YA BENKI YA EADB

 


Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), na Mawaziri wenzake wa Fedha, Mhe. Matia Kasaija (Uganda), Mhe. Ng’ongo John Mbadi (Kenya) na Mhe. Yusuf Murangwa (Rwanda) wameshiriki Mkutano wa 50 wa Bodi ya Wadhamini (Governing Council) ya Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB), unaofanyika leo tarehe 13 Machi 2025, katika Hoteli ya Serena, Kampala-Uganda.


Tanzania ikiwa moja wa nchi Wanahisa wa Benki hiyo na inanufaika kwa ufadhili wa miradi ya kimkakati na ya kijamii ikiwemo Mradi wa Reli ya Kisasa SGR pamoja na Benki hiyo kuiwezesha Sekta Binafsi ya Tanzania kupata mikopo yenye riba nafuu.


Mkutano huo umewashirikisha Wadhamini na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki hiyo wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ambaye pia ni Kamishna wa Idara ya Maendeleo ya Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Dkt. Charles Mwamwaja na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Bw. Benard Mono.

Post a Comment

0 Comments