Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Sumu Zilizobadilishiwa Matumizi Zirejeshwe haraka - AGGREY D.J.MWANRI



Na Halima Kisoma, Rufiji.

Balozi wa pamba nchini Ndug Aggrey Mwanri amewataka wakulima  waliobadilisha matumizi ya sumu ya kuua magugu kwa ajili ya maandalizi ya kilimo cha pamba na kufanyia kilimo kingine  kuzirejesha haraka,  watakaoshindwa kuzirejesha hatua za kisheria zitachukuliwa.


Hayo ameyasema Leo Ijumaa tarehe 2 August 2024  katika mkutano na wakulima wa zao hilo uliofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya serikali ya Kijiji Umwe kati, Ikwiriri Rufiji mkoani Pwani ikiwa ni sehemu ya kufuatilia Maendeleo ya kilimo hicho Cha pamba.


Barozi amewataka wakulima wa kilimo Cha pamba  kuzingatia maelekezo waliopewa awali  katika uandaaji wa mashamba, upandaji Hadi kuvuna  zao hilo la pamba ili kuweza kuvuna mazao mengi na yaliyo bora.


Aidha barozi Mwanry ametoa Rai kwa wananchi wa Wilaya ya Rufiji kuendelea kujitokeza katika kilimo Cha zao hilo walau Kila mwananchi awe amelima heka moja ya zao hilo la pamba.


Sambamba na hilo Balozi Mwanri amesisitiza  kuwa Maandalizi ya shamba yanatakiwa yaanze mapema,  ili kuweza kuzalisha pamba zenye viwango huku akiwataka wananchi kuacha tabia ya kichanganya mazao katika shamba la pamba.


Kwa upande wake mwakilishi wa kampumi ya pamba Rufiji (Rufiji Cotton) Ndug Mkono amewatoa hofu wakulima wa zao hilo kuwa pamba zote zinazozalishwa watalipa kwa wakati na hakuna mkulima atakaye chelewa kupata malipo yake au kubaki na pamba yake.


Pia Ndugu Mkono amesema kuwa kwa mashamba ya wakulima yaliyokumbwa  na mafuriko baada ya kupulizia sumu ya kuua magugu, hawatadaiwa malipo yoyote ila tu kwa wale ambao hawajapitiwa na mafuriko ndio watakao katwa  baada ya mavuno.


Nae Afisa Pamba Bi. MECKRIDA BUNDALA katika taarifa yake ya Maendeleo kwenye kata yake, amesema kuwa chanagamoto kubwa inayosumbua  wakulima kwa sasa ni mifugo kuingia  kwenye mashamba ya wakulima, huku akiimbo serikali kupitia Barozi wake kuweka kipaumbele jambo hilo ili kuweza kutatua chanagamoto hiyo.


Tani 2.5 za mbegu zimetolewa katika kata ya Umwe , ambapo Awali Eka zilizo kadiriwa kulimwa, katika kata ya Umwe ni  294, Ekari zilizopata mafuliko 80, Eka zilizolimwa 15, Ekari zilizosalimika  mpaka Sasa 15, na katika awamu ya pili (mlao)  Ekari ambazo zilitarajiwa kulimwa 94, Eka zilizo limwa mpaka sasa.


Post a Comment

0 Comments