Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Joshua Cheptegei wa Uganda ajishindia medali ya dhahabu Katika Mashindano ya Olimpiki 2024

 

Joshua Cheptegei wa Uganda ameshinda mbio za mita 10,000 kwa wanaume - medali ya kwanza kupatikana katika riadha na kuipatia Afrika dhahabu yake ya pili katika mashindano ya Olimpiki ya Paris, 2024.

Cheptegei, mshikilizi wa rekodi ya dunia wa Uganda, alitoka mbio za kufa mtu katika raundi ya mwisho na kuweka rekodi mpya ya saa 26:43.14 akitia kibindoni medali ya dhahabu ya kwanza uwanjani Stade de France.

Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 27, na bingwa wa dunia mara tatu, alimaliza mbele ya Berihu Aregawi wa Ethiopia na mshindi wa medali ya shaba Grant Fisher, wa Marekani.

Post a Comment

0 Comments