Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Dondoo Za Soka La Ulaya Kwenye Sajili Za Wachezaji

 

Tottenham hawana nia ya kumsajili Federico Chiesa, 26, kutoka Juventus licha ya ripoti kuwahusisha na mshambuliaji huyo wa Italia. (Football Insider)

Aston Villa wametoa dau rasmi kwa Sunderland kumnunua mshambuliaji wa umri wa miaka 17 Mason Cotcher. (Fabrizio Romano)

Manchester City wamekubali kumuuza mlinzi wa Finland Tomas Galvez, 19 kwa mkopo kwa mabingwa wa Austria LASK. (Teamtalk)


Inter Milan wameungana na West Ham katika mbio za kutaka kumsajili beki wa kulia Mwingereza Aaron Wan-Bissaka kutoka Manchester United, 26. (Football Insider)

Bournemouth wanamfikiria mshambuliaji wa Aston Villa Muingereza Cameron Archer, 22, kama mbadala wake iwapo mchezaji Dominic Solanke, 26, atauzwa kwa Tottenham. (Football.London)

QPR na Celtic wako katika mbio za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Liverpool mwenye umri wa miaka 21 Owen Beck. (Sky Sports)

Arsenal wanamtaka mshambuliaji wa Brighton wa Brazil Joao Pedro, 22. Football Transfers)

Fulham wanavutiwa na beki wa Aston Villa Mbrazil Diego Carlos, 31. (Mail)

West Ham wako katika mpango wa kumsajili kiungo wa Argentina Guido Rodriguez, 30, kama mchezaji huru baada ya kuondoka Real Betis. (Standard)

Mlinzi wa Villarreal Mhispania Jorge Cuenca, 24, anatazamiwa kujiunga na Fulham. (Sky Sports)

Kiungo wa kati wa Rennes Desire Doue, 19, anapendelea kuhamia Bayern Munich kuliko kusalia katika nchi yake ya asili ya Ufaransa na Paris St-Germain. (Sky Germany)


Bayern Munich imekataa dau la Manchester United mara mbili kwa mlinzi wa kati wa Uholanzi Matthijs de Ligt, 24, na beki wa Morocco, Noussair Mazraoui, 26. (Telegraph - subscription required)

Newcastle wanapanga kuanzisha mazungumzo kuhusu mkataba mpya na winga wa Uingereza Anthony Gordon, 23, atakaporejea kutoka mapumzikoni baada ya mashindano ya Euro 2024. (Athletic - subscription required)



Post a Comment

0 Comments