Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Tanzania Professional Dj's Association | MALENGO YA TPDA |

 



Kuwaunganisha DJS  wote wenye taaluma mbalimbali  nchini kuwa kitu kimoja,


 Kujenga uhusiano wa Djs ambao ni wanachama wa Tanzania Professional Djs Associational (TPDA)  na  BASATA kwa kufanya kazi kwa maslahi mapana ya  DJS kwa ushirikiano na BASATA pamoja na Wizara.


Kuhakikisha kwamba Shughuli za Djs zinaendeshwa  ili kuendana na matarajio ya  DJS kupata kipato kutokana na Kazi yake na pia kuendana na serikali yenye maono kwamba Djs anatoa mchango kwenye ukuaji wa uchumi na uzalishaji wa ajira nchini;


 Kuhakikisha DJS wa Tanzania anaendana na mahitaji ya wakati uliopo na ujao unaoongozwa na TEHAMA na unakuwa ni sehemu ya mabadiliko hayo kwa kuhakikisha kazi za Djs wa Tanzania zinanufaika na mabadiliko hayo, kutokana na namna ya kujitangaza na kupata mapato pia  Kutengeneza mbinu za kuwepo na mashirikiano (Smart Partnerships) katika kukuza sekta ya Muziki na ukizingatia utandawazi hivyo Chama kwa kushirikana na Wasanii na wadau mbali mbali wa muziki Tanzania na nje ya nchi , tutahimiza, tutahamasisha na kuratibu mashirikiano hayo baina MA DJS na Vyama vingine  na Mashirikisho ambavyo ni ya ndani au nje ya nchi kwa lengo la kukuza na kuleta ustawi kwa wanachama wetu.


Kujenga uhusiano wa kindugu kwa DJS   ambao ni wanachama wa TPDA na pia kujenga na kuimarisha Uhusiano kati ya Madjs   mbalimbali   nchini na  nje ya nchi .


Kuandaa mafunzo mbali mbali kuhusu shughuli ya DJS na maendeleo yao  kwa kushirikiana na wadau wa Muziki ikiwemo BASATA, COSOTA, Wizara na wataalam wengine mbali mbali wanaoendesha mafunzo ilikuwapa wanachama wetu na wengineo elimu kuhusu udj, masuala ya sheria za sanaa, masuala ya haki miliki/shiriki, masuala ya kodi, elimu kuhusu ujasiriamali Afya, Mazingira utalii na kadhalika kwa manufaa ya mwanachama na kazi zake; 


Kuandaa Tuzo za DJS kwa lengo la kuenzi mchango wa Madjs na kuwapa hamasa  Djs  wanachama na kizazi kipya na itasaidia kuendeleza Tasnia ya DJS Tanzania

Post a Comment

0 Comments