Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Mchezaji wa Benfica anayevutia klabu kuu za Ulaya

 

Ikiwa klabu yako itakuwekea kipengele cha kuachiliwa cha zaidi ya £100m, kwa kawaida ni ishara kuwa wewe ni mchezaji maalum. Hiyo inaweza kuwa hivyo kwa mchezaji Joao Neves, kiungo wa kati wa Benfica ambaye anatarajiwa kuhamia klabu kubwa msimu huu.


Neves, 19, ameripotiwa kuvutiwa na Manchester United na Arsenal, lakini ni Paris St-Germain ambayo inazungumziwa kuwa klabu anayoelekea kujiunga nayo zaidi.


Kijana huyo tayari ameisaidia klabu yake ya utotoni kutwaa taji la ligi na kucheza michuano ya Uropa kabla ya kufikisha miaka 20.


Je, Neves atafuata nyayo za wachezaji maarufu kama vile Bernardo Silva, Ruben Dias na Enzo Fernandez na kuwa mchezaji anayelekea kujiunga na klabu kubwa kutoka Lisbon?

Chanzo BBC Swahili

Post a Comment

0 Comments