Header Ads Widget

Responsive Advertisement

BABA MWENYE WATOTO WENGI KWENYE MGOGORO NA NETFLIX

Jonathan Jacob Meijer 


 Baadhi ya familia zinasema zilidanganywa, lakini yeye anasema kwamba hakufanya chochote kibaya, akiongeza kuwa kutoa mbegu zake kuliwapa faraja mamia ya watu.


Jonathan Jacob Meijer mwenye umri wa miaka 43 ambaye alipata umaarufu mwaka wa 2017 baada ya mahakama ya Uholanzi kumwamuru kuacha kutoa mbegu kwa kliniki za uzazi, baada ya kuzaa zaidi ya watoto 100 nchini humo pekee, ambapo sheria inaweka kikomo shughuli hiyo kwa watoto 25.


Kesi yake iliangaziwa tena mwaka wa 2023, ilipobainika kuwa hakufuata amri ya Mahakama.


Meijer aliendelea kuuza mbegu zake za kiume, na mamlaka ya Uholanzi ilikadiria mwaka huo kwamba huenda alizaa hadi watoto 1,000 kote ulimwenguni.

Post a Comment

0 Comments